Monday, July 19, 2010

Foleni za magari ni maisha bora-Rais JK

Duh huu utani sasa.Bofya hapa, najiuliza huyu matamshi haya alikuwa anatania kama kawaida wanavyotuambia au? duh! a'fu anasema mwakani anaanza kujenga bara bara za juu(flyover).

Thursday, June 24, 2010

Download the Antivirus Mixed tape ya Mr II na wenzake

Wasanii wa kibongo muda sasa wamekuwa wanalalamikia mapato madogo kutokana na kazi zao.Lawama mara nyingi ukiwasikiliza wanazitupia kwa watangazaji(Djs) wa redio au wasambazaji(wadosi) hawa kwa mujibu wasanii wamekuwa wanawapiga ganji la kufa mtu.Djs wawanaomba mlungula ili ngoma yako ichezwe redioni wadosi ndio duh!

Wasanii wakiongozwa na nguli Mr II wametoa bonge la mixed tape waliloliita antivirus wakiwavurumishia wale wanaojiita redio ya watu.Inasambazwa bure pakua hapo usikilize mwenyewe hapa

Thursday, June 10, 2010

Bringin' us promises, leavin' us poor
I heard them say, love is the way
Love is the answer, that's what they say
But look how they treat us
Make us believers, we fight their battles
Then they deceive us

-K'naan

Saturday, May 29, 2010

World Cup Afrika-Papa Afrika

Miondoko yao poa sana, bonyeza hapa

Thursday, May 20, 2010

Twitter Downtime

Mtandao wa kijamii Twitter kwa muda kidogo umekuwa chini kama unavyoonekana pichani.Mitandao ya kijamii imekuwa maarufu katika nchi za Afrika siku za karibuni baada ya gharama za matumizi ya simu kushuka kwa kiwango kidogo.

Tuesday, May 18, 2010

Kazi Microsoft na Wikipedia

Kamusi elezo ya mtandaoni Wikipedia inayotumia teknolojia katika kupashana habari na kuelimishana wamekuja na mpya.Sasa unaweza kuchangia,kupata habari kufahamu mbinu za kupata kazi kwa wanaotegemea kupata ajira Microsoft na huduma za kiMicrosoft.Bonyeza hapa usome.Angalia hapa Wikipedia ya Kiswahili

Tuesday, April 20, 2010

Bongo sijui kama tunaweza

India ni nchi moja ya maajabu sana,tangu unafika hakuishi vituko ambavyo kwa wewe mgeni vitakufanya ustaajabu kila kukicha.Ukianza na watu wenyewe mpaka chakula.

Moja ya vitu ambavyo kila siku haviishi kunistaajabisha kwa umakini wao ni uwezo mkubwa walio nao katika kutawala bara bara pasipo kusababisha ajali.Kumbuka bandiko hili nililoliweka mwaka 2006 kisha tazama video hapo chini

The most amazing bloopers are here

Unaweza kufikiri ni sinema lakini ndio hali halisi.Kwa Tanzania kitu hiki hakiwezekani,madereva nawatembea ka miguu akili zao wanazijua wenyewe.

eXTReMe Tracker