Maskini wasichana wa kidosi!
Tangu nimefika udosini kilasiku lazima iwe ni kituko au ngeni kwangu,kuanzia kwa wanizungukao mpaka matendo yao.Mfano ukija kwenye suala la mahusiano wadosi sio kama sisi.Ni watu wa kujificha ficha sana matendo yao.Ni nadra sana kukuta jinsia mbili zikitembea barabarani na hata wakiwa utaona tu wanavyojaribu kuonyesha jamii kuwa sio wapenzi.
Naambiwa naa wenyewe ukiwa na rafiki yako wa kimapenzi huruhusiwi kumleta ndani kwenye nyumba uliopangisha,mwenye nyumba ana haki ya kukuitia polisi.Na sio ajabu kuwakuta wanamalizia shida zao bustanini na kwenye migahawa.
Mara nyingi nimekuwa nawauliza kwanini pamoja na kuwa waaminifu kwa wenzi wao na wasiooa kutoruhusiwa kuwa na wapenzi iweje maambukizo ya ukimwi yapo juu kuliko sehemu nyingine ambazo mambo ni mswano tu kama Bongo? sipati jibu la uhakika zaidi ya vijana kulaani mila zao kuwa zimepitwa na wakati.
Wanawake baadhi ya sehemu udosini wanachukuliwa kama miungu,ni wasafi,watakatifu machoni mwa wanaume.Kwa hiyo sio kama bongo unampigia mluzi mwanamke utakavyo.Niliwahi kujaribu kutesti zali kumpigia mluzi msichana mmoja polisi waliokuwa karibu walisogelea na maswali kibao,nikawambia kwetu ruksa na sioni tatizo kumuita msichana hadharani kwa staili ya mluzi.
Udosini msichana akikupa namba yake ya simu hataki wengine wajue na anakupa masharti ya saa ngapi umpigie simu,baada ya hapo simu wanachukua wazazi! Ukiwauliza kama wanapenda jinsi wanavyobanwa wengi wanasema hawapendi wanavyobanwa.Ndio maaan wanapopata nafasi basi huitumia ipasavyo.
Sasa nyakati hizi udosini wanawake nawaonea huruma.Kuhalarishwa mapenzi ya jinsia moja ni pigo jingine kwao.




